Lugha

Video ya Somo la 6

Somo la 6

Ikiwa umeanza safari yako pamoja na Kristo, tumaini kwamba yuko pamoja nawe kwa sababu hivi karibuni utavunjika moyo.

Unapovunjika moyo, kumbuka kwamba Mungu ana nguvu zaidi kuliko kila kitu—pamoja na udhaifu wako. Amini kwamba anabadilisha maisha yako na kukufanya kuwa mpya.

Tunaposhindwa na kujaribiwa kuamini kuwa hatuna tumaini, tunajikumbusha kwamba tunakua, si kwa sababu sisi ni wema (sisi sio), lakini kwa sababu Kristo anafanya kazi ndani yetu kupitia imani yetu kwake, na kupitia majaribio yetu ya kumpenda, kumheshimu, na kumtii.

Je, Kristo ana uwezo wa kutosha kutuepusha na uamuzi mbaya kwa sasa? Bila shaka! Kila jambo jema maishani mwetu hutoka kwake. Mwenendo wetu mzuri unawezeshwa na yeye anapofanya kazi kupitia imani, upendo, na jitihada zetu.

Na je, yeye ni mwaminifu kukuepusha na maovu? Bila shaka lolote!

Kwa hiyo, kwa nini tunahisi kwamba hatuna uwezo? Kwa sababu anatuacha tujihisi kuwa dhaifu ili tumtegemee. Usiruhusu udhaifu wako ukudanganye. Badala yake, acha iwe sababu yako kumwamini Mungu kuwa nguvu yako.

Kwa hiyo, ni nini kinachoiba tumaini letu kwa Mungu? Tunaposhuku kwa ghafla kwamba tuna nguvu ya kutii, ni nini kilibadilika?

Tulisahau Mungu ni nani. Tulisahau kwamba sisi ni nani ndani yake. Tuliyumbayumba katika imani yetu kwamba ana uwezo wa kutosha kutuzuia tusichague uovu. Na, hatimaye, tunaiacha mioyo yetu ipotee kutoka kwake kwenda kwa vitu vingine.

Hilo kosa la mwisho ndilo la siri zaidi na ni la kudhuru zaidi. Kila kosa ovu huanza kwa kuruhusu mioyo yetu kutangatanga kutoka kwa Kristo. Ndiyo maana ni muhimu sana kusitawisha tabia ya bidii ya kusoma Biblia, kuomba, na kuabudu kila siku. Kwa sababu tunakengeushwa kwa urahisi na kumbukumbu zetu ni fupi.

Hatuwezi kusahau kuwa Mungu ndiye maisha yetu. Shairi la Wokovu linatumia maneno haya, "Badilisha maisha yangu na uyafanye kuwa mapya." Linakubali kwamba maisha yetu kamwe hayatakuwa sawa baada ya kumjua Kristo, na sababu ni asilimia mia moja kwa sababu ya utu wake.

Je! Una rafiki au mtu wa familia unayempenda kama unaukichaa? Kwa nini unampenda? Je, ni kwa sababu wewe ni mtu mzuri?

Wakati mmoja, mtu fulani alimuuliza mwanamume fulani ikiwa anampenda mke wake kwa sababu yeye alikuwa ni mtu mzuri. Jambo hili lilimfanya mwanaume huyo kuchanganyikiwa na kuchukizwa kidogo. Alimpenda kwa sababu alikuwa wa ajabu! Upendo wa mke wake kwake haukuwa na uhusiano wowote na kama alikuwa mzuri. Kwa kweli mume, alijijua kwamba hakuwa mtu mzuri, na alimpenda zaidi mke wake kwa sababu mke alimpenda licha ya ukosefu wake wa wema.

Upendo wetu kwa Yesu uko hivyo. Haihusiani na jinsi tulivyo wazuri. Tunampenda kwa sababu yeye ni wa ajabu. Kila siku, tunapaswa kufikiria sifa zake za ajabu hadi tuhisi kuhisi upendo kwake kujaa mifupa yetu kama upendo wake unajaza mifupa yetu.

Mazoea matatu yanayostawisha jambo hili ni kusoma Biblia, kuomba na kuabudu.

Je, una shaka kuwa hili linafanya kazi?

Soma ahadi za Mungu zinazohusu yeye kuto kukuacha wala kukukana. Zinazohusu ukamilishaji wa kazi yake njema aliyoianza moyoni mwako. Zinazohusu upendo wake na uchaguzi wako, licha ya chuki yako kwake. Zinazohusu uhaba wa nguvu zakututenganisha na upendo wake isipokuwa kutokuamini kwako mwenyewe na kutenda uovu wa makusudi, na kwamba amekusamehe na kukukubalia.

Unaposhuku kwamba anafanya upya nia yako, jikumbushe kwamba anafanya hivyo kupitia kutoka kwenye Neno lake. Unapotilia shaka kuwa una uwezo wa kukataa uovu, jikumbushe nyakati alizokupa nguvu za kuushinda uovu huko nyuma. Unapotilia shaka unaweza kumpenda, na kukumbuka kuwa yeye ni mzuri sana. Unapotilia shaka kwamba unaweza kufanya jambo lolote jema, jikumbushe kuwa kila jambo jema maishani mwako linatoka kwake.

Tembea kwa unyenyekevu, upendo, na utii wa vitendo kwa Kristo kwa kuamini kwamba anakubadilisha na kukufanya kuwa mpya kila mara.

Roho wa Mungu anaishi ndani yetu, akitubadilisha kwa upendo wake kwa njia ambazo huenda tusizitambue. Tunashiriki maisha yake kama vile mtoto ambaye hajazaliwa hushiriki damu ya mama yake. Mtoto na mama hubaki kuwa watu tofauti, lakini maisha yao yanachanganyika kwa njia nzuri. Vivyo hivyo, Roho Mtakatifu huzipa roho zetu uzima kwa damu ya Yesu.

Roho wake ni kile tunachohisi ndani yetu tunapoomba na kumwabudu. Hisia ya Roho wake kuishi ndani yetu ni tukio muhimu la kila siku. Bila hisia ya kudumu ya Roho wake kuishi ndani yetu, sisi ni dhaifu. Lakini pamoja naye, Roho wake hutufanya tuwe na nguvu kuliko kitu kingine chochote.

Chimbua Kwa Kina

Soma Warumi 12:1-21. Kifungu hiki kinaonyesha mabadiliko katika maisha yetu ambayo huja tunaposalimisha maisha yetu kwa Mungu kwa imani halisi. Kinatoa taswira ya jinsi upya wa kiroho unavyoonekana na kusikika. Andika na ushiriki jinsi Mungu anavyokufanya uwe mpya. Tafakari pia, je, anafanya kazi wapi zaidi kwa sasa? Tafakari jinsi anavyo kutembeza kwa subira kwenye njia ya ukuaji na ukomavu. Je, unaona uthibitisho kwamba amekuwa na neema kwako?