Lugha

Video ya Somo la 10

Somo la 10

Kanisa ni mtu yeyote ambaye ameokolewa na Mungu. Sisi ni kanisa.

Ikiwa tunasema, "Hatuhitaji kanisa," kwa uhakika tunasema, "Hatuhitaji Wakristo wengine wowote, na hatuhitaji kuwa Wakristo sisi wenyewe."

Sisi ni familia ya Mungu. Kuwa sehemu ya familia hii hutusaidia kuishi maisha ya Kikristo. Tunahitaji kila mmoja kwa sababu bila kila mmoja, hakuna familia. Bila kusaidiana katika mapenzi, tutasambaratika. Mungu alituumba tuishi naye pamoja. Ikiwa hatuishi katika jumuiya na wengine, hatutaishi kabisa.

Kama makaa ya mawe yaliyoondolewa kwenye moto, ikiwa tuko peke yetu, moto wetu utafifia. Lakini ikiwa tuko karibu na Wakristo wengine ambao mioyo yao inawaka moto, mwali wetu utazidi kung'aa.

Biblia pia inatuambia tusipuuze kukutana pamoja. Ikiwa hutakutana mara kwa mara na waumini wengine ili kusoma Biblia, kuomba, na kutiana moyo kuishi maisha ya Kikristo, hatimaye utaanguka kutoka kwa Mungu. Kuwa pamoja na Wakristo wengine kwa njia hii hutusaidia kukua; na pia inatutia moyo na kutusisimua. Inatuvuta kutoka katika asili yetu ya asili ya ubinafsi.

Hatukutani sisi kwa sisi kwa sababu tunalazimika. Tunakutana na kila mmoja kwa sababu ni zawadi kuwa pamoja. Haimaanishi kwamba tunalazimika kukutana katika nyumba za marafiki zetu Wakristo, ingawa hiyo ni nzuri na muhimu. Tunahitaji zaidi ya hayo.

Tunahitaji nini hasa?

Tunahitaji marafiki wenye upendo, wenye uwajibikaji wa kibinafsi, mafundisho thabiti, mamlaka ya Kibiblia, na fursa za kuwaongoza wengine karibu na Kristo.

Tunatakiwa kuishi chini ya mamlaka ya wachungaji na wazee ambao wamepewa vyeo vyao baada ya kuthibitisha uaminifu wao katika maisha yao na kukua kwa kweli kumjua Mungu na Neno lake. Ikiwa hatuko chini ya mamlaka ya walimu wanaostahili ambao wanaishi kulingana na yale wanayohubiri, imani yetu kumhusu Mungu inaweza kubadilika na kuwa jambo ambalo Mungu hakukusudia kamwe.

Watu wengi hawapendi kuwawajibishwa na watu wengine ili kuishi kwa njia fulani. Haliwi jambo jema kuchunguzwa maisha yetu na kuambiwa tunapovuruga na tunahitaji kubadilika. Lakini ikiwa hatutawajibika, makosa yetu yataongezeka hadi yatalipuka na kuwadhuru watu.

Kwa kuwa sehemu ya kanisa, ipo chini ya waalimu waliohitimu wanaofanana na yale yanayoonyeshwa katika Biblia, tunajiweka katika maisha ya kuwajibishwa.

Mamlaka ya waalimu waliohitimu hutulinda pia dhidi ya watu wanaotaka kuwadhulumu wengine. Inatupa watu ambao tunaweza kwenda kwao ili kupata usaidizi ikiwa tumetendewa vibaya. Mara nyingi tunahitaji mtu wa kutuunga mkono.

Hatimaye, inatupa muundo wa jumuiya ambao unaweza kupata njia ya kusaidia kuleta wengine karibu na Kristo. Hatuwezi kusahau kwamba baada ya Mungu kubadili maisha yetu, anatuagiza kuwafundisha wengine juu yake.

Ni rahisi kuinjilisha katika mazingira yasiyo na mpangilio, lakini kufuasa watu ni jukumu la muda mrefu. Daima tunapaswa kufanya watu kuwa wanafunzi huku tukijinyenyekeza kwa mamlaka ya wachungaji na wazee ambao wanaweza kutuzuia tusiwaongoze watu vibaya, au kuwaumiza watu tunaojaribu kuwasaidia.

Je, unapataje jumuiya ya waumini waaminifu? Kwanza, muombe Mungu akusaidie. Kisha uliza walio karibu. Angalia watu ambao wanaishi maisha safi, yenye upendo, na ujue ni wapi wanahudhuria kanisani. Anza kutembelea makanisa. Tafuta kanisa ambalo watu wanakaribisha, wa kweli, na wenye upendo. Tafuta wachungaji na wazee wanaoamini katika kile ambacho Biblia inafundisha kwa uwazi, na wasiwe na shaka 'na' kile ambacho Biblia inasema. Hakikisha kwamba wanachokiamini, na wanachosema ndicho wanacho ishi. Vinginevyo, hawaamini kabisa.

Kanisa lolote unaloenda, je, watu wanapendana na kutumikiana? Je, wanaipenda Biblia na kusaidiana kuishi imani yao kwa vitendo, na kwa njia halisi ambazo unaweza kuhisi na kuona? Hakuna atakayekuwa mkamilifu! Lakini unaweza kutofautisha kati ya watu ambao hawajali ikiwa maisha yao ni thabiti, na watu wanaojuta makosa yao.

Hebu jiulize swali hili: Je, Mungu anaabudiwa na kuheshimiwa hapo?

Hakuna jumuiya ya Kanisa iliyo kamilifu, kama vile hakuna watu wakamilifu. Tafuta tu kanisa linalo heshimika, nenda mara kwa mara, na usilalamike. Kuwa badiliko unalotaka kuona. Tafuta fursa za kuhimiza familia yako katika Kristo. Wapende watu kwa dhati! Tumikia upendo wako kwa moyo safi. Usifanye liwe jaribio lakuonekana tu, kama mtu “mzuri” mbele za watu wengine.

Tambua kwamba sisi ni binadamu, na kwamba tunahitajiana. Huwezi kujua, mtu anayekuudhi anaweza kuwa ni mtu ambaye Mungu amemweka katika maisha yako ili kukusaidia kukua. Na unaweza kuwa umewekwa katika maisha yao ili kuwasaidia kukuza upole wao katika Kristo. Ishi kwa amani, pamoja na kumheshimu Mungu. Hilo ndilo kanisa.

Chimbua Kwa Kina

Tafuta kanisa na uhudhurie Jumapili hii ijayo. Andika mawazo yako kuhusu tukio hilo, na jinsi lilivyokugusa kihisia, kiroho, na kimwili.