Lugha

Video ya Somo la 7

Somo la 7

Mungu anatoa zana zenye matokeo katika vita vyetu vya kuishi kwa ajili yake. Bila kuzitumia, tutashindwa.

Maisha ni magumu. Ukristo sio imani inayokuficha ili usiumie. Badala yake Mungu amewasha moto mioyoni mwetu na kutuamuru kumulika moto huo katika giza tulimozaliwa. Anatuambia tuishi maisha yetu halisi, tofauti na mienendo ya maisha yakidunia.

Tunapozaliwa mara ya pili, tunahitaji kulishwa mara kwa mara kwa maisha yetu yote. Tunakula mara kadhaa kwa siku. Tunalala masaa mengi kwa siku. Tunakunywa maji mengi kwa siku. Mazingira mbadala ya kiroho, ya chakula, maji na usingizi, yanahusu, kusoma Biblia, kuomba, na kuabudu, pamoja na wengine.

Dunia ni chafu. Tunatakiwa kuwa wasafi. Tunapoishi, tutakuwa na uchafu kwenye mioyo yetu kila siku. Kupitia macho yetu, tunaona upotovu. Kupitia masikio yetu, tunasikia laana. Kupitia mikono yetu, tunasikia maumivu ya miiba na ngumi za marafiki. Kupitia ndimi zetu, tunaonja sumu chungu. Kupitia pua zetu, tunanusa uozo wa kifo.

Je, ni zana gani ambazo Mungu hutupa ili kuosha uchafu, kurudisha giza nyuma, na kubadilisha ulimwengu unao tuzunguka?

Kwanza, kama tulivyokwisha zungumza, alifunua mpango wake wa maisha yetu katika Biblia. Kwa kusoma maandishi ya Biblia na kuthamini ahadi za Mungu, ndani, tunatakaswa akili zetu na mioyo yetu kuimarishwa.

Pili, ameweka Roho Mtakatifu ndani yetu, ili tuweze kumuomba Mungu na kuhisi anajibu kuomba kwetu. Hii inakuza ukubali wetu na kutupa uwezo wa kuishi tofauti na kusaidia kubadilisha ulimwengu.

Tatu, alituumba kwa ajili ya ibada. Tunapomwabudu, yeye hutosheleza tamaa zetu, na kuanza kuponya majeraha ambayo ulimwengu huu unatupa.

Nne, alitufanya tufurahie na kupenda watu, wanyama, na ulimwengu ambao ametupa ndani ya mipaka. Tunahitaji kutanguliza kuwa pamoja na watu wengine na kufurahia ulimwengu wa asili.

Tunahitaji kutanguliza utumishi wa wakati pamoja na watu wengine wanaomwamini Mungu na kumpenda jinsi tunavyofanya. Hili hututia moyo na kututia nguvu. Linatuzuia kupata hali ya kujihisi kutokuwa na usawa. Hili linaitwa kanisa. Kanisa si jengo tunalokutana ndani yake au ibada tunayohudhuria; kanisa ni watu wanaompenda Mungu na kupendana wao kwa wao. Kutumia wakati pamoja na watu wengine wanaompenda Mungu (kusoma Biblia, kusali, kuabudu, na kusaidiana kuishi jinsi anavyotuambia tuishi katika Biblia) ni muhimu.

Wengi wamejiuliza kama kukutana na Wakristo wengine inaumuhimu. Lakini Biblia inasema ni jambo lililo la lazima. Yesu alifufuka tena ili kujenga jumuiya yenye upendo: iliyotakaswa ndani yake na kuridhika naye. Alionyesha hilo katika tabia yake baada ya kufufuka kutoka kwa wafu alipokula pamoja na marafiki zake, kutembea nao, na kuwatembelea katika vyumba vyao na faragha.

Ikiwa hiyo haitoshi kwetu, hadithi hii ya uchochezi ambayo kasisi alituambia inaweza kusaidia:

Siku moja, mtu mmoja alikuja kwa kasisi na kusema, “Baba, ndugu yangu, Paulo, amejitenga na mimi na kila Mkristo mwingine. Unahitaji kwenda kuzungumza naye na kumshawishi maana anapaswa kurudi!”

Kasisi alienda kwenye nyumba ya Paulo, akabisha hodi, na kuambiwa aingie.

Akiwa ndani, alimkuta Paulo akiota moto uliokuwa ukiwaka. Waliitikia kwa kichwa salamu za kimya, na kasisi akaketi karibu na Paulo na kuutazama moto. Baada ya muda kidogo, kasisi akaokota koleo la chuma, akachukua makaa meupe ya moto kutoka kwenye moto, na kuyaweka kwenye sakafu ya mawe nje kidogo ya moto. Alitikisa kichwa kwa Paulo, akatabasamu, na kusubiri. Baada ya dakika chache, makaa ya mawe yalipoa sana mpaka ayakuwa na moto uliobaki.

Kasisi huyo alimpungia Paulo kwa kichwa, akachukua makaa, na kuyatupa tena ndani ya moto. Baada ya dakika chache, makaa ya mawe yalikuwa yanawaka tena. Kasisi huyo alicheka, akamtikisia kichwa kwa mara ya mwisho Paul, na kuinuka ili kuondoka.

Sisi ni makaa hayo. Bila moto wa wengine unaowaka karibu nasi, tutapoa hatimaye na kupoteza moto wetu. Tunahitaji kusoma Biblia zetu, kukuza tabia za kila siku kuwa za bidii ya maombi na ibada, na kutanguliza kutumia wakati wa pamoja na Wakristo wengine, ili tusaidiane kuishi kwa furaha, na kumtii Mungu.

Tukifanya hivyo, Mungu atatuimarisha, atatutia moyo na kutubariki. Kisha atatupatia fursa za kushiriki, Injili na watu wanaoihitaji sana kama sisi.

Chimbua Kwa Kina

Soma Wagalatia 5:22-26, Zaburi ya 121:1-8, na 1 Wakorintho 12:20 - 13:13. Je, hili ni wazi kwako kuhusu jinsi Mungu anavyotaka tuishi? Omba Mungu akupe nguvu ya kuishi kwa upendo unaosoma katika mistari hii. Ni njia gani moja wapo unayoweza kuanza kuweka upendo wa aina hii katika vitendo? Iandike, kisha uende ukafanye!