Lugha

Video ya Somo la 3

Somo la 3

Jambo la msingi zaidi katika tumaini letu ni kujua kwamba Yesu alifufuka kutoka kwa wafu na yuko hai milele. Ingekua kwamba Yesu bado yupo kifoni, tusingeweza kuona maisha yake. Lakini Roho wake anayeishi ndani yetu ni mojawapo ya zawadi kuu zaidi anazozitoa.

Maisha yetu pamoja na Mungu yanawezekana kwa sehemu, kwa sababu kifo chake kilitufanya tuwe safi machoni pake, lakini maisha yetu ya wokovu yanafanywa kuwa halisi kwasababu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu na kuishi milele mbinguni na ndani yetu. Hivi ndivyo tulivyoahidiwa kuishi milele baada ya kufa, kwa sababu tutavuliwa maisha yetu yaliyovunjika na kubakiwa na maisha yake tu yasiyo na mwisho.

Yesu ni Mungu kweli, na mwanadamu kweli. Adamu na Hawa, mwanamume na mwanamke wa kwanza, waliumbwa waishi milele, lakini maamuzi yao mabaya yaliwaua. Uovu ndio utakaotuua pia. Tunakufa kwasababu ya uovu lakini Yesu anaishi milele kwa sababu hakuwahi kufanya jambo lolote baya. Hii inaonyesha kwamba alikuwa Mungu, kwa sababu Mungu pekee ndiye mkamilifu.

Ingawa Yesu alikufa, uovu haukumuua. Alitoa maisha yake kwa hiari, na kifo hakikuweza kumshikilia kwa sababu hakuwahi kufanya kosa. Usafi wake wa moyo ulimpa haki ya kuchukua maisha yake tena.

Kwa hiyo, ndivyo alivyofanya.

Yesu alifufuka, akionyesha uwezo wake, umungu, ubinadamu mkamilifu, na uwezo wa kutupatia uzima na kutufufua kutoka kwa wafu. Lakini zaidi ya hilo, alifufuka ili tuishi kwa urafiki wa karibu naye milele.

Hebu tufikirie hili kidogo.

Hatupaswi kuwa wapweke kamwe kwa sababu Yesu anaishi ndani yetu. Tunaweza kumfikia kila dakika ya kila siku. Tunaweza kumuomba na kuhisi hisia zake zikichochea mioyoni mwetu. Anajua mawazo yetu na anatupenda. Anatupa uwezo wa kuishi maisha safi. Tunaweza kuishi katika upendo wake, furaha, amani, subira, fadhili, wema, uaminifu, upole, na kiasi. Anatupatia uzima kwa ukamilifu zaidi, tunapopata uhai wetu ndani yake.

Biblia inasema kwamba sababu yetu ya kuwepo ni kuishi katika uhusiano wa ukaribu pamoja na Yesu. Kuishi karibu naye kuliko mtu mwingine yeyote kwenye sayari yetu. Kumpenda yeye kuliko kitu chochote au mtu mwingine yeyote. Na kumtii kwa furaha na kumwabudu milele.

Kwa sababu tunaishi ili kumpenda Yesu na kuishi pamoja naye, Biblia inawaita Wakristo “bibi-harusi wa Kristo.” Biblia pia inasema kwamba yoyote anayemkana amehukumiwa. Hatima yetu ni kuwa katika mikono ya Yesu. Hakuna mtu anayemchukia Yesu atakayeishia mikononi mwake; badala yake, atatenganishwa naye milele.

Hii ni hofu ambayo wachache wanaweza kufikiria. Si wengi wanaotambua kwamba maisha au furaha yoyote tuliyo nayo hutoka kwa Mungu. Katika maisha, tunaweza kupata raha rahisi kwa sababu yeye ametupatia. Tunapokufa, hayo yote yatavuliwa, ama tutabaki na Yesu kwa furaha isiyo na mwisho, au, kinyume cha hapo, ambacho ni hofu ya utengano na uchungu.

Tunaanza kuona kwamba mikono ya Yesu ndiyo mwisho mkuu zaidi katika ulimwengu. Ukweli ni kwamba tunaweza kupata amani na maisha pamoja naye sasa, ambayo ndiyo furaha kuu maishani. Mtu yoyote ambaye ameishi kwa ukaribu wa kweli na Yesu, atakuonyesha kuwa Yesu ni bora kuliko kila kitu.

Hapo awali, kuacha aishi nafsini mwetu, tunaweza kuhisi hofu, kwasababu anaangaza uovu wetu na kutusukuma kutubu. Lakini tunapojisalimisha, yeye huleta uponyaji mtamu na kutupa nguvu za kustahimili na kukua.

Ukimfuata Yesu na kujisalimisha kwake, atakuwa furaha yako kuu, na atabadilisha maisha yako na kukutakasa.

Kisha, baada ya kufa, utaingia katika Paradiso mikononi mwake.

Chimbua Kwa Kina

Soma Warumi 1:1-7, 1 Wakorintho 15:1-5, na Warumi 10:9-10. Haya ni maelezo kuhusu ufufuo baada ya ufufuo kutokea. Kisha soma Danieli 12:2, Ayubu 19:23-27, Isaya 26:19-21, Hosea 6:1-2, Hesabu 21:9 (pia soma Yohana ya 3:14-15 ili kupata maana ya kumbukumbu hii), Zaburi ya. 16:9-10, na Zaburi ya 71:19-24 . Hayo ni maelezo kuhusu ufufuo wa Yesu na wale wanaokufa wakiwa waaminifu kwake, yaliyoandikwa muda mrefu kabla ya Yesu kuja duniani. Andika maana ya ufufuo wa Yesu kwako, na kwa nini unafikiri kufufuliwa kwake kutoka kwa wafu ni muhimu kwaajili ya maisha yako. Ikiwa una maswali, pata muda uzungumze na Mkristo mwingine.